NINI MAANA YA URAFIKI.
Kwa ufupi na kwa maneno
rahisi; Urafiki ni uhusiano mzuri kati ya watu wawili au zaidi.
Kwa kufafanua zaidi, Urafiki
ni uamuzi wa binafsi wa mtu, kuchagua uhusiano wa karibu na mtu mwingine
kutokana na misimamo na haja za moyo wake. Urafiki ni kujitoa au kuji-commit (commitment) kwa mwengine au
wengine kutokana na uamuzi wa binafsi wa moyoni mwa mtu huyo kulingana na
misimamo, machaguo na haja za moyo wake katika maisha yake.
KWANINI TUNAHITAJI MARAFIKI?
1. Kujaza hitaji la binadamu la
kupendwa na kupenda. (Math 22:37-39)
Kila mtu ameumbwa na haja
ya kupenda kutambulika na kuthaminika. Urafiki unatupa kujisikia kupendwa na
kujaliwa na kutabulika. Usipokuwa na marafiki, utasikisikia kutothaminika.
2. Kujaza hitaji la kibinadamu
la kushirikiana, kusaidiana na kuchangamana. (Mhu 4:9-10)
Hakuna mtu
ameumbwa kujitosheleza mwenyewe tu kwa mahitaji ya kimwili kiroho na kiakili. Hakuna
mtu anayejua kila kitu wala hakuna mtu anayeweza kufanya kila kitu. Ndio maana
Biblia inasema tunafahamu kwa sehemu tu (1Kor
13:9). Mtu huwezi kuishi kama kisiwa peke
yake. Tumeumbwa na mapungufu ambayo yanaweza kujazwa na watu wengine.kwaababu
hiyo, tunahitajiana. Urafiki unatupa kuchangamana na kushirikiana maisha
yetu na wengine. Kuna wakati wa kila jambo chini ya jua. Maisha yamejaa nyakati
za furaha na taabu pia. Marafiki wanatusaidia kuwa nasi nyakati zote.
3. Kuweza kuwafahamu watu na
kujifahamu mwenyewe.
Kuchangamana na watu
katika urafiki na ushirika mbalimbali, kunatupa kuwafahamu watu wengine tabia
zao, mienendo yao, fikra zao, maisha yao n.k. Kuwajua watu
kunakuwezesha kujijua na wewe pia, kwamba moyo ukoje (haupendi mambo/vitu fulani
na unapenda mambo gani)
4. Kujifunza na kujiendeleza
kitabia, kiakili na kiroho.
Ni marafiki wanaoweza
kutusaidia kuwa watu wazuri zaidi kitabia kwa kutubadilisha mienendo isiyofaa.
Ni marafiki wanaotufundisha maarifa na elimu mbaimbali. Pia ni marafiki
wanaoweza kutusaidia kukua kiroho na kumjua Mungu zaidi.
5. Kwa ajili ya kupata
mwenzi wa maisha. (Mwa 2:8,18)
Kati ya watu tunaowafahamu
na kukutana nao katika maisha ya kila siku, Mungu atakupa mwenzi wa maisha
(mume au mke). Ni muhimu kufahamiana vizuri kabla ya kuingia katika nadhiri za
kuoana, kwasababu maisha mazuri ya furaha na amani, huwafuata watu wanaoendana,
wanaoelewana na wanaofanana. Urafiki unakupa kuwafahamu watu na kati ya hao,
utakutana na mwenzi wako wa maisha.
AINA ZA MARAFIKI
1. PEER FRIENDS (Marafiki wa mbali) *Luke 6:14-17
Ni wale marafiki
tunaokutana au kushirikiana nao mambo ya kawaida ya kila siku.
2. CASUAL FRIENDS (Marafiki wa kawaida) *Luke 10:1,17-20
*Math 10:1-8,;
Ni wale
tunaopenda kuwa nao katika vitu tunavyopenda kuvifanya. (Company)
3.
CLOSE
FRIENDS. (Marafiki wa karibu) *Math 17:1-9 *Mith 18:24 *Luk 8:50-51
Ni wale
tunaopenda kuwashirikisha siri na mambo yetu ya muhimu sana.‘best friends’.
4.
INTIMATE
FRIENDS. (Marafiki wa moyoni) *Yoh 10:30 *Math 26:36-44
Ni
yule mmoja na wapekee ambaye umempa moyo wako wote na maisha yako (mpenzi)
Aweza
kuwa - Rafiki Mpenzi, Rafiki Mchumba au Rafiki Mwanandoa.
5. MENTOR
FRIENDS (Marafiki walezi) * Kut 24:12-18 *Kut 33:7-11
Ni
wale marafiki waliotutangulia kwa umri au uzoefu au maarifa ya kimaisha na
kiroho. Urafiki ulio katikati yenu ni wa kulea, kufunda, kufunza maarifa ya
kimaisha na kiroho. (1Tim 1:2)
SIFA NA TABIA ZA
MARAFIKI WAZURI
1.
Anakufahamu/Anakujua. (He/She knows you and knows about you.)
Ahafahamu majina yako, historia yako, ndugu zako, matakwa yako, mipango
yako, nk.
2. Anapenda kuwa nawe (He/She loves your
presence)
Anapenda na anatafuta muda wa kukutana
nawe (company).
3.
Anawasiliana nawe (Communicates)
4. Anakujali na Anakusaidia (Cares
and gets concerned)
5. Anakuheshimu na kukuthamini (Respect and
Honour)
6. Anakuvumilia/Anachukuliana nawe (Patient and
Barerence)
7. Anakuwa Mkweli na Mwaminifu (True and
Faithful)
8. Anakurekebisha na Anakuonya (Corrects and
Worns)
9. Anajitoa na ni Mtoaji kwako (Sacrifice and
Giver)
10. Anakuamini na kukutegemea
(Trust and Dependance)
AINA ZA UPENDO.
1. UPENDO AGAPE - UPENDO WA MUNGU. (Godly Love) Rum 5:8 Yoh 3:16
Agape ni aina ya
upendo wa ki-Mungu, utendao kazi
ndani ya mtu pasipo masharti yoyote au
Mfano; Upendo wa
Msamaria mwema. (Luka 10:29-37)
Sifa kuu tatu (3) za Upendo wa ki-Mungu (Agape).
i.
Hauangalii hali ya mtu ya nje.
ii.
Hauna masharti yoyote ya kupenda.
iii.
Hauna kipimo au kiwango cha kupenda.
iv.
Hauna mwisho au kikomo cha kupenda.
2. UPENDO PHILEO – UPENDO WA KIRAFIKI. (Friendship
Love)
Phileo
(Kiebrania) ni upendo wa
kirafiki. Phileo ni upendo wenye
sababu. Kiingereza wanasema ‘congitional
love’. Ni upendo wenye sababu. Huu ndio upendo unaokuwepo kati ya marafiki.
Yohana 14:21,23. Mithali 8:17
Mfano; Urafiki
wa Jonathan na Daudi. (1Samweli 18:1-4)
Urafiki wa Yesu na Lazaro, Mariam na Martha.
(Yohana 11:5, 35-36)
Sifa kuu tatu (3) za Upendo wa kirafiki (Phileo).
i.
Unaangalii hali ya mtu ya nje.
ii.
Una masharti yoyote ya kupenda.
iii.
Una kiwango au kipimo cha kupenda.
iv.
Una mwisho au kikomo cha kupenda.
3.
UPENDO EROS –
UPENDO WA KIMAPENZI AU MAHABA. (Romantic/Sexual Love)
Eros ni upendo wa kimapenzi au kimahaba unaokuwa kati ya
watu fulani kusababisha watu hao kuwa na uhusiano wa kimapenzi (mahaba) kati yao. Kwa utaratibu wa
Mungu na jamii zilizo ‘sawa sawa’, Eros ni
aina ya upendo unaotakiwa kuwa kati ya watu wenye uhusiano wa ki-ndoa, yaani
mtu mke na mume au kati ya watu wanaoelekea katika uhusiano wa ki-ndoa wa mume
na mke. (Waefeso 5:25; Mhubiri 9:8-9;
Wimbo Ulio Bora 7:1-10; Wimbo Ulio Bora 4:1-7)
Mfano;
Upendo wa Yakobo kwa Raheli. *Mwanzo 29:16-20 (10-30)
Upendo wa Isaka kwa mkewe
Rebecca. (Mwa 26:1-11)
Sifa /
Baadhi ya Dalili za Upendo Kimapenzi (mahaba) Eros.
1)
Mvuto kwa Haiba yake na kuchukuliana nayo.
(Mwonekano na tabia).
2)
Kukaa mawazoni kwa mtu anayependa. (Kujaa moyoni)
3)
Shauku kubwa ya kuwa pamoja kila wakati.
(Kuambatana)
4)
Heshima kubwa kwa mtu apendwae (Utii na Uaminifu)
5)
Kumjali na kumtanguliza mtu apendwae. (Kipaumbele)
6)
Zawadi na gharama kwa mtu apemdwae.
(Kujitoa/Sacrifice)
7)
Furaha na Amani kutawala moyoni. (Kuridhika)
4.
UPENDO STORGE –
UPENDO WA KIFAMILIA. (Family Love)
Upendo storge
ni upendo wa kifamilia, ni upendo unaotokana na damu moja ya undugu.
Mfano; Upendo wa
Musa kwa Mwebrania mwenzake. (Kutoka 2:11-12)
Upendo wa Baba kwa Mwana mpotevu. (Luka
15:11-32)
Upendo wa
kindugu, storge unafanana kwa sehemu na ule upendo wa ki-Mungu
wa agape.
- Hauangalii hali ya nje ya mtu.
- Hauna masharti ya kupendwa.
- Hauna kikomo au mwisho wa kupendwa.
Tofauti yake
moja kubwa na upendo wa agape ni
kwamba, upendo wa kindugu una kiwango
au kipimo cho kupenda. Ndugu wanapendana lakini kwa viwango tofauti; upendo wao
haulingani. Tofauti ningine kubwa ni kwamba, kwasababu huu upendo wa kindugu unatokana na binadamu, basi ni
lazima hautakosa madhaifu mengi.
NAMNA YA KUPATA
MWENZI MZURI WA MAISHA.
(HOW TO FIND/GET A GOOD MARRIAGE PARTNER)
*Mithali 19:14, 21
1. Mweleze Mungu vizuri, zile haja za moyo wako. (Mwa
2:18)
Mungu anaheshimu
sana haja za
moo wako ambazo zitakupa wewe furaha ya maisha.
(Mathayo 7:7-11; Wafilipi 4:6-7 ; Zab 145:17-18) Hii ni
kwasababu, Mungu anaheshimu sana
matakwa na mahitaji ya watoto wake, maana anapenda kuiona furaha ya watoto
wake.
Isa 45:11 ; 1Kor
7:39; Yak :16, Luk 18:1, Kol 4:2.
2. Mwombe Mungu akuonyeshe au akukutanishe na mwenzi
wako. (*Yer 33:3)
Kumwomba Mungu
kusababisha mazingira ambayo yatawakutanisha na mtatambuana baada ya kupata
ufahamu wa Mungu kwamba ‘you belong together’ yaani mnaendana, mnafanana,
mnafaana na hivyo mnaweza kuishi pamoja vizuri. Hiyo ndiyo maana halisi ya
kufunuliwa au kuonyeshwa. Japo Mung5 anaweza kukupa maono katika ndoto au
katika maombi, lakini si lazhma iwe hivyo. Si kila mtu anaweza kupata maono
kuhusu mwenzi wake. Soma Efe 1:15-19, Jab 32:,
Isa 43:26, Isa 45:11
3. Tengeneza marafiki. (*Mith 18:24, Mith 17:17)
Watu wengi
humwomba Mungu kwa uaminifu sana
ili wapate mwenzi wa maisha. Lakini wanfanya makosa ya kujifungia katika kisiwa
cha upekee. Ni ngumu sana kuOnekana na
kujulikana tabia na utu wako wa ndani kama
hudachangamana na jumuiya za ma2afiki. MunGu ndiye chanzo cha urafiki. Hat Yesu
alikuwa na marafiki wa kiume na waki kike pia. (Yoh 11:5). Jithidi kufanya marafiki mvalimbali ila
mwombe Mungu akupe marafiki wazuri. Mk 5:25 – (30) – 34; inasema, wengi
walimgUsa Yesu na kumsUkuma-sukuma, lakini ni mmoja tuambaye atakuwa na mguso
wa tofauti katika moyo wako.
ISHARA ZA KUTAMBUA (UPENDO WA) PENZI LA
KWELI.
1.
Mtu huyo atakamata umakini wako na atakuvutia
(attention).
2.
Atajaa moyoni na mwazoni mwako kuliko kawaida na
wengine.
3.
Utatamani sana
uwepo wake wakati wote (kuwa naye).
4.
Utapenda kuwasiliana naye mara kwa mara (kama hamko wote).
5.
Utakuwa na moyo wa kumjali, wema, zawadi na kujitoa sana kwa ajili yake.
6.
Utakuwa na heshima ya juu sanA,
adabu, uTii na uaminifu sana
kwake.
7.
Utakuwa na maneno mazuri, maneno laini, na maneno ya
upendo kwake.
8.
Utakuwa na moyo/uwezo wa kumvumilia au kuchukuliana
naye vile alivyo.
9.
Utakuwa na hamu ya kumgusa au kumshika kwa upendo (si
tamaa).
10. Utakuwa
na moyo na utayari wa kumlinda Na kumhifadhi.
11. Uhusiano wenu
utapendeza mbele za watu wengi (si lazima wote)
12. Utakuwa
na amani na furaha ya ajabu moyoni mwako/mwenu.
Mungu
alisema kwa mkono wa Mtume Paulokuuelezea Upendo kwA namna hii;
1 Cor 13 :
4-8(a)
*
Upendo huvumilia/subira (Love is patient)
*
Upendo hufadhil)/hufania wema (Love is kind)
*
Upendo hauna husuda (Love doesn’t Envy)
*
Upendo haujivuni (Love is not proud)
*
Upendo haukosi adabu (Love is not rude)
*
Upendo hauna ubinafsi (Love is not selfish)
*
Upendo hauna uchungu (Love is not easily angered)
*
Upendo hauhesabu mabaya (Love doesn’t count wrongs)
*
Upendo haufurahii uovu (Love doesn’t rejoice with
evil)
*
Upendo hufurahia ukweli (Love rejoices in truth)
*
Upendo unalinda (love always protects)
*
Upendo huamini yote (Love always trusts)
*
Upendo hutumaini (Love always hopes)
*
Upendo hustahimili (Love always perseveres)
5. Omba
ushauri kwa watu wanaokujua/wanaomjua huyo umpendaye.
2Kor 13:1; Zab
73:24; Mith 15:22
Ushauri kutoka
kwa watu werevu wanaomjua Mungu na wanaowajua ninyi wawili utakuhibitishia
kwamba ulichsikia mooni juu ya huyo mtu ni sahihi. Mashauri ya watu yanaweza
kukusaidia kufanya maamuzi magumu nay a muhimu.
(Math
18:16; 1Tim 5:19; Ebr 10:28; Fil 4:6-7, Kol 3:15 na Isa 55:12
6. Mwendee
na Useme naye kwa hekima. (*Wimbo 3:1-4)
Baada ya maombi
na subira, Mungu akuongoze kusema naye kwa wakati utakaoongozwa na Mungu. Uwe
jasiri na muwazi. Lakini usemi wako uwe wa kawaida (simple). Usichague maneno
magumu wala misamiati wala mafumbo. Uwe wazi na wa kawaida.
7. Thibitisha
uhusiano wako/wenu (kiofisi). (*Wimbo 3:4)
Baada ya kuongea
na kulitafakari pamoja kwa muda mtakaoona unatosha au unafaa, ni muhimu sana sasa mpelekane mbele,
katika mamlaka zenu za kifamilia na kikanisa. Uhusiano mzuri usiwe wa
mafichoni. Tunaona huyu mpenzi katika kitabu cha Wimbo anasema, anataka
kumtafuta mpenzi wake, amshike mkono, wapelekane kwa wazazi. Huo ndio utaratibu
mzuri kibiblia. Familia na kanisa watawasaidia kufuata taratibu za kiutamaduni
na kiroho ili mhalalishwe kuwa mume na mke. Ndipo ndugu na marafiki
mtawashirikisha mipango yote ili kuandaa harusi na maka